Ufalme usiotetemeka
An Unshakeable Kingdom (Swahili)
mafundisho juu ya barua kwa Waebrania
Barua kwa Waebrania inatukumbusha maneno makubwa juu ya Bwana wetu Yesu Kristo - uungu wake, umutu wake, ufufuko wake toka wafu, kwenda kwake mbinguni, na ya kwamba atarudi tena. Lakini kuna maonyo mengi vilevile ndani ya barua hii. Mbele ya kuanza kusoma na kueleza barua hii tuone kwanza kama iliandikwa kwa watu gani, kwa wakati gani, na kwa sababu gani. Kujua maneno haya kutatusaidia kufahamu nini Mungu anataka kutufundisha sisi kwa njia ya barua hii, na roho zetu zitafurahishwa na maneno ya ajabu tutakayosoma juu ya Bwana wetu Yesu Kristo. Kutatusaidia vilevile kupokea maonyo ya barua hii kwa sisi wenyewe na kuyanyenyekea. Haifai tujifurahishe na maneno matamu tu tunayoyasoma ndani ya Biblia bila kuwaza na kunyenyekea maonyo yanayoandikwa ndani yake kwa sisi. Tukumbuke ya kwamba barua kwa Waebrania ni sehemu ya Neno la Mungu lisiloweza kugeuka kamwe.